• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

HALMASHAURI YA TUNDURU YAWAFIKIA VIJANA BODABODA NA BAJAJI, YAWAFUNGULIA MILANGO YA FURSA ZA KIUCHUMI.

Imewekwa : February 4th, 2026

Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imefanya ziara ya kutembelea vijiwe vya maafisa usafirishaji wa bodaboda na bajaji, ikiwa ni sehemu ya juhudi za Serikali kuwafikia vijana na kuwaelimisha kuhusu fursa mbalimbali za maendeleo zilizopo katika eneo lao.


Katika ziara hiyo, maafisa maendeleo ya Jamii walitoa elimu kwa vijana kuhusu fursa za kiuchumi ikiwemo mikopo ya asilimia 10 (10%) inayotolewa na Halmashauri kwa vikundi vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu. Vilevile, vijana walielimishwa kuhusu fursa za mikopo ya vyombo vya moto, zikiwemo pikipiki na bajaji, inayotolewa na Benki za NMB na CRDB kwa masharti nafuu.

Aidha, Halmashauri ilitumia fursa hiyo kuwajulisha vijana kuhusu upatikanaji wa mafunzo ya muda mfupi ya udereva yatakayotolewa na Chuo cha Ufundi Nazareth Mbesa, Tawi la Tunduru Mjini (Biasi). Mafunzo hayo yanalenga kuwawezesha vijana kupata vyeti vya udereva na hatimaye kumiliki leseni halali ili wawe madereva rasmi wanaotambulika kwa mujibu wa sheria.


Pia, ziara hiyo ililenga kusikiliza na kupokea changamoto pamoja na maoni kutoka kwa vijana, ikiwa ni utekelezaji wa adhma ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ya kuwafikia vijana, kuwasikiliza na kushughulikia changamoto zao ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.


Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imeendelea kuwasisitiza vijana kutumia fursa zinazotolewa na Serikali ili kujikwamua kiuchumi na kuchangia katika maendeleo ya Wilaya na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • WAZEE WATAJWA NGUZO YA MAENDELEO: MWENYEKITI HALMASHAURI YA TUNDURU AZUNGUMZA NA WAZEE WA WILAYA.

    February 04, 2026
  • HALMASHAURI YA TUNDURU YAWAFIKIA VIJANA BODABODA NA BAJAJI, YAWAFUNGULIA MILANGO YA FURSA ZA KIUCHUMI.

    February 04, 2026
  • TAARIFA KWA UMMA

    February 04, 2026
  • MKURUGENZI MARANDO AAGIZA MIRADI YOTE IKABIDHIWE IFIKAPO TAREHE 01 MACHI, KAZI IFANYIKE USIKU NA MCHANA.

    February 03, 2026
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.