• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Elimu Tunduru

Imewekwa : February 14th, 2018


Haya yalisemwa na Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh. Juma Z.Homera katika kikao cha tathimini ya Elimu wilaya kilichofanyika katika ukumbi wa klasta ya mlingoti Tunduru Mjini, ikiwa ni pamoja na kuweka mikakati ya kiwiliya ya kuinua kiwango cha ufaulu Tunduru.

Akifungua kikao cha tathminiya elimu Wilayani Tunduru kilichohudhuriwa na wadau wa elimu kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya ya Tunduru Mkuu wa Wilaya ya Tunduru  Juma Homera alisema kwamba katika matokeo ya kidato cha nne mwaka 2017 Halmashauri ya Tunduru imeshika nafasi ya tano kati ya Halmashauri nane za mkoa wa Ruvuma na katika nafasi za kitaifa wilaya ya Tunduru ni ya 179 kati ya Halmashauri 185.

Mkuu wa wilaya Juma Homera aliendelea kusema kuwa ili kuboresha kiwango cha ufaulu katika wilaya ya tunduru idara ya elimu msingi na sekundari iandae mitihani kwa kidato cha nne , pili na darasa la saba kila baada ya miezi 3 ili kuwapima wananfunzi kila mara na kuwajengea uwezo.

Pia alitoa maagizo kwa watendaji kata, vijiji na Maafisa Elimu Kata kufuatilia idadi ya wanafunzi waliojiandikisha darasa la kwanza na awali ambao bado hawajaripoti shuleni na wale wa sekondari wasioripoti shuleni mpaka sasa ili  wazazi au walezi kuchukuliwa hatua.

Mwenyekiti wa huduma za jamii ambaye pia ni diwani wa Kata ya Ligoma Mh. Abasi Ngajime akitoa mchango wa kuberesha mazingira ya watoto ambao wazazi wao wanaenda kufanya shughuli za kilimo mbali na mazingira ya kijiji ili weweze kuapata fursa na haki kupata elimu kwani ni haki yao.

 “Watendaji wa Kata, Vijiji na Maafisa Elimu kata fuatilieni taarifa za kuandikisha wanafunzi wa awali na darasa la kwanza  na watoto wote wenye  umri wa kuanzia miaka 4-5 waende shule na mfanye kazi kwa nafasi zenu kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma na msisubiri kusukumwa” alisema Juma Homera.

Afisa Elimu anayeshughulikia wanafunzi wenye mahitaji maalum mwalimu Albart akipokea maagizo kutoka kwa mkuu wa Wilaya ya kuandaa mahitaji wa wanafunzi wenye mahitaji maalum ili serikali iwezeshe ununuzi wake kupitia mfuko wa Elimu Tunduru.

Aidha akitoa ufafanuzi wa upungufu mkubwa wa miundombinu ya shule katika Halmashauri ya wilaya Tunduru, mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa katika msimu wa korosho wa mwaka 2017/2018 serikali ilianzisha mfuko wa kuchangia elimu na kukata wakulima wa zao la korosho katika kila kilo moja ya korosho sh 30 na zaiadi ya  milioni 600 zimekusanywa.

“Niwaombe walimu mtuandalie vipaumbele vya mahitaji ya upungufu wa miundombinu ikiwa ni pamoja na  nyumba za watumishi, matundu ya vyoo, vyumba vya madarasa katika shule za msingi na sekondari.” alisema Juma Homera

wadau wa elimu wilaya ya Tunduru wakifuatilia kikao cha tathmini ya elimu wilaya kilichofanyika katika ukumbi wa Klasta ya Mlingoti

Na kwa upande wa  wadau wa elimu wilayani Tunduru walishauri kwa pamoja mambo yafuatayo yakifanyika kiwango cha elimu kitaongezeka na kufikia malengo ya kuondoa daraja sifuri kabisa.

Kuanzishwa kwa klabu za midahalo (debates), michezo na makongamano ya wanafunzi kati ya shule na shule ili wanafunzi kuweza kubadilishana uzoefu na pia katika kila shule kuwa na majaribio ya mara kwa mara, pamoja na morning speeches, vitu ambavyo vitawajengea uwezo wa kujiami wanafunzi na kujifunzi lugha ya kiingereza.  

Afisa Taaluma akisoma taarifa ya Elimu Taaluma  Mwalimu Mussa Chandu katika kikao cha Tathimini ya Elimu Wilaya.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.