• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Elimu bila malipo, mtoto aende shule kila mdau awajibike

Imewekwa : May 7th, 2018

Akisoma taarifa ya mgawanyo wa vifaa vya ujenzi kwa mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi.Christina Mndeme, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Tunduru ndg Chiza Cyprian Marando amesema kuwa halmashauri ilianzisha mkakati wa kuondoa changamoto ya miundombinu ya shule kwa kila kijiji kuwa na benki tofali laki moja (100,000) katika mwaka wa fedha 2016/2017, ili kuhakikisha sera ya  elimu bila malipo inafanikiwa kwa kuwashirikisha wadau  wa elimu.

Katika kutekeleza kauili mbiu ya "Elimu bila malipo, mtoto aende shule kila mdau awajibike" halmashauri ya Tunduru ilianza kwa kuwashirikisha wadau wa elimu katika msimu wa zao la korosho mwaka 2017/2018 kwa kuanzisha mfuko wa elimu, ambapo kwa hiari ya wakulima wa Tunduru walikatwa  shilingi 30 kwa kila kilo moja ya korosho.

Fedha hizi zilipelekwa moja kwa moja katika kuboresha miundombinu ya shule na jumla shilingi  milioni 608,248,680.00 zilikusanywa  “tumefanikiwa kununua malighafi za ujenzi kutoka viwandani kwa bei ya jumla ili kupunguza gharama, vifaa vyenye thamani ya milioni 225,251,040 ambayo ni saruji mifuko8720,bati 3132, na nondo 880 na kuokoa shilingi milioni 36,516,000 ambazo zinaweza kujenga hosteli moja na kukamilika” alisema mkurugnzi mtendaji halmashauri ya Tunduru ndg Chiza Marando.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi.Christina Mndeme akitaka utepe katika uzinduzi wa zoezi la ugawaji wa vifaa vya ujenzi (aliyevaa Blauzi ya Blue) uliofanyika Nakayaya katika ghala la kuongeza thamani zao la mchele terehe 06/05/2018

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Tunduru mh juma zuberi homera wilaya ya Tunduru ina shule za msingi 150, ikiwa 149 ni za serikali na moja ya mtu binafsi na shule za sekondari 23 ikiwa 21 ni za serikali na 2 ni za watu binafsi.

Pia alisema halmashauri ya wilaya ya Tunduru ilikuwa na changamato kubwa ya miundombinu ya elimu, na kufikia hatua ya kupanga mikakati na wadau zao la korosho kuwakata wakulima shilingi 30 kwa kila kilo ya korosho ili kuweza kujenga miundombinu ya shule na kuhakikisha kuwa madarasa ya nyasi wilayani Tunduru yanakwisha.

mkuu wa mkoa wa Ruvuma bi. Christina Mndeme akifuatilia taarifa ya uzinduzi wa mgawango wa vifaa vya ujenzi na Elimu wilayani Tunduru iliyokuwa inasomwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Tunduru ndg Chiza Marando.

Akihutubia wananchi na watendaji waliohudhuria katika uzinduzi wa kugawa vifaa vya ujenzi wa miundombinu ya elimu vyenye thamani ya shilingi milioni 225,251,040 mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi Christina Mndeme aliwataka watendaji kuziogopa fedha hizo za elimu kama kimeta kwani watafuatilia na kufanya ukaguzi wa namna zitakavyotumika.

Aliendelea kutanabaisha kwa Maafisa elimu Kata, wakuu wa shule na Walimu wakuu, watendaji wa Kata na waheshimiwa madiwani, bodi za shule na kamati za ujenzi za shule kufanya usimamizi wa kila siku ili kuhakikisha kuwa fedha hizo zinatumika kwa malengo kusudiwa.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bi Christina Mndeme (wa tatu kutoka kushoto) akiwapongeza viongozi wa halmashauri ya wilaya ya Tunduru kwa ubunifu wa kutatua changamoto za elimu, baada ya kufaya zoezi la uzinduzi la ugawaji wa vifaa vya ujenzi vyeneye thamani ya shilingi milioni 225,251,040 wa wakuu wa shule za mchangani, umoja ambao waliwakilisha shule zingine zenye mradi wa ujenzi kupitia fedha za mfuko wa elimu wa zao la korosho mwaka 2017/2018.

Aidha Bi Mndeme alisema aliagiza kwa shule ambazo wamepelekewa miradi hiyo kuwa anatoa muda wa miezi mitatu ili kuhakikisha kuwa ujenzi umekamilika. “ninaomba shule zote zilizopokea miradi kuhakikisha kuwa ndani ya miezi mitatu ujenzi umekalimika, kama ni darasa, nyumba ya mwalimu, hosteli au matundu ya vyoo view vimekamilika ili kuboresha mazingira ya kufundishia na kusomea kwa wanafunzi”

Hata hivyo mkuu wa mkoa aliwataka watendaji kuwa waaminifu na kufanya kazi ya usimamizi kwa weledi na kuepuka tamaa na kuhakikisha kuwa vifaa hivyo inasafirishwa na kufikishwa katika shule bila ya ubabaifu na kuepukana na udanganyifu kwani serikali haitosita kuwachukulia hatua za kisheria na kinidhamu.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.