• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Tunduru ataka ushirikiano kutoka kwa wananchi kesi za Unyanyasaji kijinsia wanawake na watoto

Imewekwa : March 8th, 2019

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh Juma Zuberi Homera katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yenye kauli ya Badili fikra kufikia usawa wa kijinsia kwa maendeleo endelevu, katika sherehe hizo zilizofanyika katika viwanja vya baraza la Idd wilayani Tunduru .


Mh.Homera ameitaka jamii kutoa  na ushirikiano na jeshi la polisi kwa kutoa  taarifa za uhalifu na unyanyasaji wa wanawake na watoto unaofanywa katika familia, ikiwa ni pamoja na wanaume kuwalawiti watoto wa kuwalea, masuala ya mirathi na maendeleo katika familia.


Alisema "imekuwa ni kawaida kwa wanaume wengi kutumia mabavu hasa pale wanaposhauri na wake zao masuala ya maendeleo, na badala yake huwakatili wake zao kuamua  kuongeza au kuoa mke mwingine, ili kuepuka hayo wanawake wengi wananyamaza kimya ili kulinda ndoa na kushindwa kudai haki zao dawati la jinsi polisi liko wazi"

Mkuu wa wilaya alisema kumekuwa na tabia ya wananchi kutotoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa taarifa za wahalifu waliopo katika maeneo yao, akitoa mfano wa mkazi mmoja wa Kata ya Majengo wilayani Tunduru aliyekuwa anajihusisha na biashara haramu ya kusafirisha wanafunzi wa sekondari kuwapeleka katika nchi jirani kufanya kazi za ndani na uchimabji wa madini, hali wazazi wanakaa kimya bila ya kutoa taarifa kwa vyombo husika.

"niwatake waalimu wote kufanya ufuatiliaji wa wanafunzi katika mahudhurio shuleni ili kubaini na kudhibiti utoro na kama ukiona mwanafunzi hajahudhuria shule zaidi ya wiki basi chukua hatua za makusudi, ufuatiliaji uanze mara moja ili kunusuru mabinti wetu wanajiingiza katika mambo yanayokatisha ndoto zao" alisema mkuu wa wilaya ya Tunduru.


wanawake wakiwa katika maandamano kueelekea katika uwanja wa baraza la Idd ambapo  maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kiwilaya yamefanyika

Serikali imeboresha sekta ya elimu wilayani Tunduru kwa kuanzisha shule ya kidato cha kwanza hadi sita ya masonya sekondari na nandembo sekondari kidato cha tano na sita lakini pia kuna mikakati ya kuanzisha shule nyingine za wasichana ili kuwanusuru watoto wanaokatisha masomo kutokana na kupata mimba mashuleni.


Naye mwenyekiti wa halmashauri ya Tunduru mh.mbwana mkwanda sudi ambaye pia ni diwani wa kata ya Mchoteka aliwaomba wazazi kutoa mkazo katika elimu ya watoto wao hasa wa kike.

Aidha aliwaasa  wanawake kuacha kubagua na kuchagua baadhi ya kazi na kusema hizi ni kazi za wanaume, pia kufanya marejesho ya mikopo ili asimilia 10 ya mapato ya ndani inayotengwa na halmashauri iwanufaishe wanawake wengi zaidi na kupunguza umaskini.


Akitoa elimu ya kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto mwakilishi wa dawati la jinsia kutoka jeshi la polisi  Tunduru ndg Tumaini Msowoya alitoa ombi kwa walimu kuwa marafiki wa wanafunzi badala ya kutumia viboko kama sehemu ya adhabu tuu pale mwanafunzi anachelewa shule au kuwa mtoro, kwani kufanya hivyo kutajenga urafiki na wanafunzi hivyo kujua changamoto nyingizinazowakabili.

Takwimu za kiwilaya zinaonesha mimba za utotoni kwa kipindi cha mwaka 2018  pekee jumla ya watoto wenye umri wa chini ya miaka 18 3277 wamejifungua katika hospitali ya wilaya ya Tunduru, kati yao 38 walipoteza maisha na 50 kujifungua kwa upasuaji.

katika picha ni wanawake wajasiamali wa wilaya ya Tunduru wakimsikiliza mgeni rasmi ambaye hayuko katika picha wakati akitoa hotuba kwenye maadhimishi ya siku ya wanawake duniani iliyofanyika katika viwanja vya bazara la Idd Tunduru.

"hali hii ni mbaya sana kwa wilaya yetu kwani changamoto ya wafanyakazi na viongozi wanawake itaongezeka kwani ni kundi kubwa sana la watoto wanaacha kufikia malengo na ndoto zao, wazazi fanyeni majukumu yenu mnapoenda mashambani kulima muwaachieni watoto wenu vyakula ili wasiingie kwenye vishawishi vya mimba za utotoni"alisema bi mwageni.

Hata hivyo maadhimisho hayo yalipambwa kwa bidhaa mbalimbali kutoka katika vikundi vya wajasiriamali wanawake ndani ya wilaya ya Tunduru, naye mgeni rasmi pamoja na wageni wote walipata fursa ya kuona kazi zinazofanywa na vikundi vinavyowezeshw ana halmashauri ya Tunduru, huku wakioomba kuletewa wakufunzi wa kutoa mafunzo ya ili kuongeza kasi ya uzalishaji.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.