• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Mtatiro azungumza na wananchi Tunduru

Imewekwa : January 30th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Wakili Julius S. Mtatiro ameongea na wananchi wa Tunduru kupitia mkutano ya hadhara  tarehe 29.01.2024 uliondaliwa katika tarafa ya Matemanga. Mkutano huo ulilenga kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi wa haraka.

Pichani: Baadhi ya wanakijiji wa Matemanga wakiwa katika Mkutano wa Hadhara.

Akizungumza katika mkutano huo Mhe. Wakili Mtatiro alisema kazi kubwa ya watumishi wa serikali ni kuwafikia wananchi ili kusikiliza kero na kuweza kuzitatua kwa kuzipatia suluhisho la kudumu. Sambamba na hilo, Mhe. Wakili Mtatiro aliwasisitiza wananchi kuwapeleka watoto shuleni.

Pichani: Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Wakili Mtatiro akizungumza na wananchi.

“Niwaombe wanajami, pelekeni watoto shuleni, hakuna maendeleo yatakayokuja kwa kuuza korosho pekee, hakuna kinachoendelezwa bila elimu” Alisema “Tutakaa tunalalamika kila siku kuwa hatupigi hatua kwenye maendeleo yetu pamoja na kwamba tunapata mazao ya kutosha, jamii itatoka kwenye umaskini pale ambapo elimu itathaminiwa”

Pichani: Wananchi wa Tarafa ya Matemanga wakitoa kero zao mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Wakili Mtatiro.

Aidha, Katika mkutano huo aliwasisitiza wananchi juu ya kuongeza mashamba ili kuweza kuongeza tija kwenye mazao. Pia, aliendelea kuwasisitiza wananchi kukodisha mashamba badala ya kuyauza ili kusaidia kupunguza migogoro ya ardhi na ufugaji wa mifugo kiholela.

“Tuwekeze  nguvu kwenye kuandaa mashamba vyema yawe kwenye ubora ili uzalishaji wa mazao uwe juu, hii pia itasaidia kuongeza faida, kila unapohudumia shamba lako kikamilifu tarajia kupata mazao ya kutosha. Ni vigumu kuzuia mtu asiuze shamba lake lakini ni vizuri sana apewe elimu kabla ya kufanya maamuzi hayo” Alisema “Wakulima wengi hawajui siri ya kufanikiwa katika mazao hasa korosho, siri kubwa ni kuongeza mikorosho mipya ili kuweza kupata faida ya uhakika”.

Ziara hiyo ya Mkuu wa Wilaya imekuwa ya mafanikio makubwa kwani ameweza kusikiliza kero za wananchi mmoja mmoja na kuweza kuzitatua kwa wakati. Wananachi walipata wasaa wa kuelezea kero, hoja na mapendekezo yao ambayo walisaidiwa na kupatiwa ufumbuzi.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.