• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Mtatiro atoa maagizo kuchochea maendeleo na kuimarisha kilimo Tunduru.

Imewekwa : November 2nd, 2023

Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mheshimiwa, Wakili Julius S. Mtatiro alihudhuria baraza la madiwani la robo ya kwanza kwa mwaka wa fedha 2023/2024,Novemba o1,2023 katika ukumbi wa klasta-Mlingoti , ambapo ameelekeza nakutoa maagizo yanayolenga kuimarisha maendeleo.

Katika maagizo yake, Mh. Wakili Mtatiro aliagiza Miradi yote ya maendeleo ikamilike kwa wakati, pamoja na kuwepo changamoto kadhaa, aagiza wataalamu na wasimamizi kuzifanyia kazi haraka iwezekanavyo ili ikamilike na wananchi waanze kupata huduma.

Kuhusu kilimo, Mh. Wakili Mtatiro alitoa maelezo juu ya mbolea. Alisema, kutakuwepo na mfumo utakaomwezesha mkulima kupokea mbolea bila kupoteza muda na kutumia gharama kubwa za usafiri. Maelekezo haya yataleta tumaini kwa wakulima walioko vijiji vya mbali.

“Utaratibu wa viuatilifu umekamilika, tumekutana na makampuni tumepanga mpango kazi, nimeruhusu kampuni hizo kukutana na ushirika pamoja na vyama vya ushirika” Alisema. “Mbolea itakua kwenye ghala, na wananchi watakuwa wakikusanya fedha zao za mbolea kwenye AMCOS, kampuni hizi zitakuwa zikichukua mbolea na kuipeleka kwa mkulima mahali alipo, gharama za kupandisha na kushusha zitakua juu ya kampuni, lengo ni kuondoa gharama kwa mwananchi kusafiri toka vijiji vya mbali kufuata mbolea mjini”.

Akizungumza katika Baraza hilo, aliagiza pia ufugaji holela kukomeshwa kwani ardhi ya Wilayani Tunduru ni kwa ajili ya kilimo, alisema, ufugaji holela unasababisha uharibifu wa mazingira na kuzorotesha uzalishaji wa mazao, wafugaji waende maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya shughuli hiyo.

Maagizo hayo ya Mkuu wa Wilaya yanalenga kuboresha hali ya maisha,Ukamilishaji wa miradi ya maendeleo utaleta fursa na utasaidia katika upatikanaji wa huduma bora, Kukomesha ufugaji holela kutasaidia kulinda ardhi ya wananchi wa Tunduru. Pia, upatikanaji wa mbolea kwa urahisi hasa kwa wananchi waishio vijijini utasaidia kuongeza tija katika kilimo.

Imeandaliwa na Orpa Kijanda, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.