• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC MASANJA akabidhi hati 472 za kimila kwa wakazi wa kijiji cha Ngapa; Ataja faida zake katika kuondoa migogoro ya ardhi.

Imewekwa : August 12th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa Denis Masanja, amekabidhi hati za kimila 472 kwa wananchi wa Kijiji cha Ngapa. Mpango huu una lengo la kuleta utulivu na maendeleo kwa jamii. Utekelezaji wake unalenga kuondoa migogoro ya ardhi na kuimarisha usalama wa umiliki wa ardhi miongoni mwa wananchi, ambao mara nyingi wamekuwa wakikumbana na changamoto mbalimbali.

Akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Ngapa, Dc Masanja alielezea kwamba, upatikanaji wa hati hizi unawaongezea wananchi ulinzi wa kisheria wa ardhi zao. Hati miliki za kimila zinatambulika kisheria, na hivyo kumpa mmiliki uwezo wa kudai haki zake endapo ardhi yake itavamiwa au kutumiwa na mtu mwingine bila ridhaa yake. Hii itawapa wananchi uhakika na amani ya moyo kwamba mali zao ziko salama na zinalindwa na sheria.

“Moja ya faida kubwa ya mpango huu ni kutatua migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikiwakabili wakulima, wafugaji, na maeneo ya hifadhi. Kwa kuweka mipaka wazi na kurasimisha matumizi ya ardhi, zoezi hili linazuia mwingiliano usio wa lazima na hivyo kupunguza uwezekano wa kutokea kwa mizozo” Alizungumza DC Masanja “ Kupitia hati miliki za kimila, kila mwananchi anajua eneo lake na matumizi yake yamerasmishwa, jambo linalochangia amani na utulivu katika jamii zetu”.

Faida nyingine muhimu ni kwamba hati hizi zinaweza kutumika kama dhamana katika taasisi za kifedha, kama vile benki na taasisi nyingine za mikopo. Kwa kuwa na hati miliki ya ardhi, wananchi wanapata fursa ya kukopa fedha na kuanzisha au kukuza miradi yao ya maendeleo. Hii inachochea ukuaji wa kiuchumi kwa ngazi ya mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla.

Aidha, Hati miliki pia zinatoa fursa kwa wamiliki kuzitumia kama dhamana mahakamani kwa ajili ya kesi mbalimbali, isipokuwa kesi za jinai. Hii inawasaidia wananchi kuwasaidia wapendwa wao katika matatizo ya kisheria bila kupoteza mali zao nyingine. Utoaji wa hati hizi unafungua milango ya fursa nyingi za kiuchumi na kijamii kwa wananchi.

Akitoa taarifa kwa Mkuu wa Wilaya, ndg Stephen Mpondo Afisa Mahusiano Jamii kutoka Hifadhi ya Taifa Nyerere (W),alizungumza kwamba, Jumla ya hati 2,783 zimetayarishwa kwa ajili ya vijiji nane vilivyopo katika Wilaya ya Tunduru vyenye mipango ya matumizi ya ardhi, kupitia mradi wa ERB unaosimamiwa na Hifadhi ya Taifa ya Nyerere. Kati ya hati hizo, Kijiji cha Ngapa pekee kimepokea hati 472. Vijiji vingine vilivyofaidika ni Muhuwesi (hati 291), Mnazi Mmoja (hati 355), Liwangula (hati 312), Chawisi (hati 225), Jaribuni (hati 314), Matemanga (hati 156), na Ligunga (hati 658). Mpango huu unaonesha dhamira ya serikali ya kuboresha maisha ya wananchi wake kupitia urasimishaji wa umiliki wa ardhi.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.