• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC MASANJA AFANYA KIKAO NA TANAPA KUJADILI MIKAKATI YA KUIMARISHA MASUALA YA UHIFADHI TUNDURU.

Imewekwa : October 22nd, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mhe. Denis Masanja ameongoza kikao cha tathmini na kupanga mikakati mipya ya kuimarisha uhifadhi na kupunguza migongano kati ya binadamu na wanyamapori, kilichofanyika kwa ushirikiano na Wakala wa Huduma za Wanyamapori Tanzania (TANAPA).

Kikao hicho kimejikita katika  kutathmini utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Shirika kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2020/21. Ambapo mafanikio na changamoto za kiuhifadhi ziliainishwa ikiwa ni pamoja na uharibifu wa mazao na Mali za wananchi unaosababishwa na wanyamapori husisani katika vijiji vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Nyerere pamoja na vile vilivyopo katika ushoroba wa Selous-Niasa

Miongoni mwa yaliyopendekezwa ni pamoja na:

1. Kutoa elimu endelevu kwa jamii kuhusu namna bora ya kuishi kwa amani na wanyamapori na kutatua migongano bila kutumia nguvu.

2. Kuwezesha mipango ya matumizi bora ya ardhi ili kuzuia uvamizi wa maeneo ya wanyama na binadamu.

3. Kuimarisha doria za pamoja (joint patrols) kati ya TANAPA, Halmashauri na vyombo vya ulinzi ili kudhibiti ujangili na uharibifu wa mazingira.

4. Kujenga vituo vya kudumu vya PAC katika vijiji vinavyoathirika zaidi.

5. Kuongeza vitendea kazi kama magari, ndege ndogo za doria, na helikopta kwa ajili ya kudhibiti wanyamapori waharibifu.

6. Kuendeleza ushirikiano na jamii kwa kuajiri na kutumia Vijana wa Gawio la Uhifadhi (VGS) ili wajisikie sehemu ya jitihada za uhifadhi.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Masanja alisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano kati ya wananchi na taasisi za uhifadhi, akisema kuwa maendeleo endelevu hayawezi kupatikana bila uhifadhi imara wa mazingira.

Aliongeza kuwa Serikali itaendelea  kuhakikisha migongano kati ya binadamu na wanyamapori inapunguzwa au kuondolewa kabisa, huku jamii ikinufaika na rasilimali za uhifadhi.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.