• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Homera apongeza wananchi Nasya kushiriki ujenzi wa zahanati ya kijiji

Imewekwa : April 17th, 2019

Aliyasema hayo katika mkutano wa hadhara wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi uliofanyika katika kijiji cha Nasya mapema wiki alipofika kukagua eneo lililotengwa kwa ajili ya kujenga zahanati ya kijiji hicho.

Akisoma taarifa ya kijiji hicho afisa mtendaji wa kijiji hicho alisema ujenzi wa zahanati hiyo ulianza mwaka 2012 kwa kutenga eneo lenye ukubwa wa ekari nne, na kuanza kumwaga jamvi na jumla ya shilingi milioni 11 zilitolewa kupitia mfuko wa jimbo katika awamu mbili kwa mwaka 2012 na mwaka 2016.

Aliendelea kusema kuwa wananchi wameendelea kupata tabu ya kutembea umbali mrefu kufata huduma katika zahanati ya kijiji cha Tuwemacho na kituo cha afya Mtina, huku wakikumbana na changamoto kubwa hasa kipindi cha masika.

Akizungumza na wananchi mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Zuberi Homera alianza kwa kuwapongeza wananchi kushiki kikamilifu katika kuanzisha ujenzi wa zanahati hiyo, huku akitoa ahadi ya mifuko 100 ya saruji kwa ajili yakuendeleza ujenzi huo.

katika picha ni wanachi wa kijiji cha nasya Kata ya Tuwemacho Kijiji cha Nasya wakiwa katika mkutano wa Hadhara na Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mh. Juma Zuberi Homera ulifanyika tarehe 16/03/2019 


"mimi nitachangia mifuko mia moja ya saruji kwa ajili ya kuendeleza ujenzi na wananchi nawaagiza kukusanya mchanga kutoka mto Msenjewe, kila kitongoji mpangiane ratiba ya kwenda kuopoa mchanga mtoni"alisema mkuu wa wilaya ya Tunduru Juma Homera.

Sambamba na hayo Mkuu wa Wilaya aliutaka uongozi wa kijiji hicho kutunza eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya kwa kuzungushia uzio ili kuepkuka uvamizi unaofanywa na watu wasiokuwa na huruma wananchi hasa kinamama wanaosafiri umbali mrefu kufata huduma za afya.

Juma Homera alisema kuwa kukamilika kwa ujenzi wa zahanati ya Kijiji cha Nasya kutaondoa changamoto ya huduma za afya kwa kinana na watoto kwa kusogeza huduma karibu na wananchi lakini pia kupunguza vifo vya mama na mtoto kutokana na kutembea umbali mrefu kupata huduma katika vijiji vya Mtina na Tuwemacho.

Kwa upande mwingine Afisa afya Ndg Ayubu Joseph Majumbawima aliwataka wanawake wajawazito wanapojigundua mara ni wajawaziti kuanza kliniki mara moja ili kupata dawa za kumkinga mtoto na malaria , vyandarua na kupima afya pamoja na wenza wao.

Diwani wa Kata ya Tuwemacho Mhe.Hadija Timamu akieleza changamoto za wananchi wa kijiji cha Nasya katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini tarehe 16/03/2019

Ayubu aliendelea kusema kuwa ili kutokeza malaria katika kijiji cha naysa ni vyema wananchi wakazingatia usafi wa mazingira kwa kuvyeka nyasi katika kijiji na maeneo yanayozunguka nyumba zao kwani hayo ndio masalia ya mbu wanaoeneza malaria.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.