• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Chacha, Aagiza Wanafunzi kupata Mlo Shule.

Imewekwa : May 7th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Mheshimiwa Simon Kemori Chacha, amewaagiza viongozi katika kata na vijiji, pamoja na maafisa elimu kata kuhakikisha wananfunzi wanapata mlo wakiwa shuleni wakati wa masomo.

Amesema kuwa kufanya hivi kutaongeza ufanisi na umakini kwa wanafunzi katika masuala ya elimu, hasa katika kuongeza uelewa pale wanapofundishwa na walimu wao.

“Lishe ni kitu muhimu sana katika maisha ya kila mwanadamu , tunatakiwa kulichukulia hili suala kwa uzito wake katika maeneo yetu tunayoishi”.Alisema Chacha.

Chacha alitoa agizo hili wakati wa kikao cha tathmini ya utekelezaji wa mkataba wa afua za lishe ngazi ya wilaya. Kikao hicho kilihudhuriwa na watendaji wa kata pamoja na wataalamu kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Aidha, Mkuu wa Wilaya alisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya viongozi wa kata na vijiji, maafisa elimu, na jamii kwa ujumla katika kuhakikisha wanafunzi wanapata mlo bora shuleni. Alisema kuwa ushirikiano huo utasaidia kufanya kazi ya kuendeleza lishe bora katika Wilaya ya Tunduru.

Afisa Lishe wa Wilaya ya Tunduru, Ndugu, Martin Kigosi, aliwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa lishe wilaya na jamii kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2024. Alisema kuwa wilaya imefanikiwa kutekeleza viashiria vya mkataba wa lishe kwa mwaka wa fedha 2023/2024 kwa asilimia 93.1 robo ya kwanza, asilimia 96.7 robo ya pili, na asilimia 96.3 robo ya tatu.

Kigosi alipongeza jitihada zilizofanywa na viongozi wa kata na vijiji, maafisa elimu, na jamii kwa ujumla katika kutekeleza mkataba wa lishe. Aliwataka waendelee na jitihada hizo ili kuhakikisha Viashiria vyenye alama ya kadi nyekundu vinaondoka katika Wilaya ya Tunduru.

Kikao hicho kilimalizika kwa wito kwa viongozi wote kuhakikisha utekelezaji wa mkataba wa lishe kwa ufanisi zaidi. Inaaminika kuwa mlo bora kwa wanafunzi utasaidia kuboresha ufanisi wao katika masomo na hatimaye kuleta maendeleo kwa wilaya na taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.