• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

DC Tunduru Atoa kilio cha Tatizo la Mimba mashuleni kwa wazee.

Imewekwa : October 1st, 2019

na Theresia Mallya                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                      01/10/2019

Tundurudc.

Tatizo la Mimba mashuleni katika shule za sekondari wilayani Tunduru limekuwa changamoto kubwa sana katika utoaji wa huduma za elimu mashuleni licha ya jitihada zinazochukuliwa na serikali katika kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunza bado kuna nguvu ya ziada inatakiwa kuchukuliwa katika kutokomeza suala hilo.

Haya yamesemwa kwa masikitiko makubwa na mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe. Julius Mtatiro mapema leo wakati akizungumza na wazee wa wilaya hiyo katika maadhimisho ya siku ya wazee Duniani yenye Kauli mbiu inayosema "Tuimarishe Usawa Kuelekea Maisha ya Uzeeni" ambaye alikua mgeni rasmi.

Akitoa takwimu za Mimba kwa wanafunzi wa sekondari kwa kipindi cha miezi Miwili ya Agosti na Septemba Mkuu huyo wa wilaya amesema kuwa jumla ya wanafunzi 43 wamekatisha masomo wakiwa ni wa kidato cha kwanza hadi cha nne, ikiwa katika ya hao wanafunzi 25 walipatikana na mimba kwa kipindi cha mwezi Agosti pekee  na mwezi agosti ni wanafunzi 19 hivyo kufanya jumla kuwa 43. Idadi hii ni kubwa sana kwani inaeudisha nyuma jitihada za serikali katika sekta ya elimu.

Baadhi ya wazee wa wilaya ya Tunduru wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Tunduru Mhe. Julius Mtatiro wakati akitoa hotuba katika maadhimisho ya siku ya wazee duniani ambayo yamefanyika kiwilaya katika ukumbi wa Klasta ya Mlingoti Mapema Leo.

Ameendelea kuwaeleza wazee kuwa kwa kipindi cha miezi 9 yaani kuanzia Januari hadi kufika julai 2019 jumla ya wanafunzi wa kike 119 wamekatisha masomo sababu ya kupata ujauzito angali bado wako shuleni, lakini kati ya kesi zote 119  Takwimu zinaonesha kuwa kesi nane tu ndio zilizofikishwa Mahakamani huku kesi nyingine 111  wazazi wakizimaliza wenyewe huko mitaani lakini kwa kipindi cha januari hadi septemba jumla ya wanafunzi wa kike waliokatisha masomo ni 162.

Julius Mtatiro ameendelea kusema  kuwa sababu kubwa ya kuwa na wimbi la Mimba nyingi kwa wanafunzi ni watoto kukosa uangalizi wa wazazi kwani jamii inawaacha watoto kujihudumia wenyewe hasa kipindi cha kilimo wanaenda mashambani na kuwaacha peke yao nyumbani,wazazi kutojali wanafunzi wanapopata Mimba na mila na desturi hasa Unyago unachangia kwa kuwa na ongezeko kubwa la Mimba mashuleni.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe.Julius Mtatiro akisalimiana na Wazee alipofika katika ukumbi wa klsata mapema leo katika maadhimisho ya siku ya wazee duniani.

Vilevile wazazi na jamii kutozingatia maadili na malezi ya watoto nayo imekuwa ni chanzo kikubwa cha watoto kupata mimba angali bado wanafunzi. amesema "kati ya kesi 25 za mwezi Agosti watuhumiwa 16 wamefikishwa mahakamani h kufunguliwa jalada n zinaendelea katika mahakama ya wilaya huku watuhumiwa  15 kati ya 19 za  mwezi septemba  wamefikishwa mahakamani kwa kosa la kuwatia wanafunzi Mimba, wazazi 6 wamefikishwa mahakamani kwa kushirikiana na watoto kutoa Mimba kwa kipindi cha mwezi agosti, huku zikiripotiwa zaidi ya kesi 3000 za utoaji Mimba kwa watoto katika kipindi cha Januari -Decemba 2018.

hata hivyo amewaomba wazee kufanya kazi ya malezi na maelekezo katika jamii kwani wazee ni hazina ya Taifa, pia kutoa mkazo katika elimu kwani maendeleo hayawezi kuja pasipo kuwa na elimu, hivyo amewaomba wazee na jamii ya Tunduru kwa Ujumla kuwekeza katika Elimu na kuachana na mila na desturi potovu ambazo zinawaiingiza mabinti wengi wadogo katika kupata mimba wakiwa bado wanahitaji kupata Elimu.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.