• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Tunduru District Council
Tunduru District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Vision and Mission
  • Utawala
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maliasili na Utalii
      • Ushirika
      • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
      • Usafi na Mazingira
      • Mipango,Ufuatiliaji na Takwimu
      • Utawala na Usimamizi wa Rasilimali watu
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Sheria
      • Manunuzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Mawasiliano Serikalini
      • Michezo,Utamaduni na Sanaa
    • Muundo wa Taasisi
  • Fursa za uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Biashara na Viwanda
    • Mining
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Huduma za Watumishi
    • Elimu
      • Elimu ya awali na elimu msingi
      • Elimu Sekondari
    • Kilimo,Mifugo na Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha za Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
      • Huduma za Jamii
      • Kudhibiti Ukimwi
      • Maadili
    • Time Table
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Tarajali
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Fomu
    • Machapisho
    • Mkataba wa Huduma kwa wateja
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Picha
    • Video
    • Habari

Bazara la Biashara

Imewekwa : November 21st, 2017


Baraza la Wafanyabiashara Tunduru Laanzishwa.

Baraza la wafanyabiashara ni chombo kilichoundwa kisheria kwa waraka wa Rais Na 1 wa mwaka 2001 na kuchapishwa katika Gazeti la serikali Na.691 tarehe 28 septemba mwaka 2001 ikiwa na lengo la kuunda jukwaa la majadiliano kati ya sekta binafsi na sekta ya Umma katika kila ngazi ya utawala ili kujadiliana jinsi ya kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji.

Baraza la biashara lipo katika utaratibu wa kisheria kwani mwenyekiti wa baraza la kitaifa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk John Pombe Magufuli, katika ngazi ya mkoa ni mkuu wa mkoa na katika ngazi ya wilaya mwenyekiti wake ni mkuu wa wilaya husika.

Baraza hili limelenga katika kuboresha maeneo sita ya uboreshaji wa mazingira ya biashara katika matokeo makubwa sasa ambayo ni kuangalia upya mfumo wa kisheria na kitaasisi, Upatikanaji wa Ardhi na uhakika wa umilikishaji, Usimamizi na Uratibu wa shughuli za biashara, Utitiri wa kodi, tozo, na ada, Kuzuia na kupambana na Rushwa, sheria na stadi za kazi na Usimamizi wa mikataba na sheria za kazi.

Akiongea katika mkutano wa ufunguzi wa baraza la wafanyabiashara wilaya ya Tunduru mwenyekiti wa halmashauri Mh.Mbwana Mkwanda Sudi alisema wilaya ya Tunduru ina fursa nyingi sana za uwekezaji katika sekta ya Biashara, Kilimo, Afya, Elimu, Uchumi, utalii.

Mwenyekiti Mkwanda Sudi alisema katika sekta ya Utalii wilaya ya Tunduru ina vivutio vingi vya utalii ambavyo havijaendelezwa na endapo sekta binafsi itashiriki kikamilifu sekta ya utalii unaweza kutengeneza ajira za kutosha kwa jamii ya Tunduru na kufungua milango ya maendeleo katika wilaya yetu.

“Tunduru kuna nyao za viumbe vyote vinavyoishi duniani ambayo katika jiwe huko njenga ambayo naifananisha na safina ya Nuhu, kuna masalia ya majengo ya wapigania uhuru wa Msumbiji ya Masonya, vifuko alivyotumia Rais wa kwanza wa Msumbiji Samora Machel, Sultan Mataka na misafa ya watumwa wakitokea Msumbiji hadi Kilwa katika kipindi cha ukoloni na mengine mengi ambayo yanahitaji kuendelezwa” alisema mwenyekiti

Aidha meneja wa tanesco wilaya ya Tunduru Ndg Joseph K. Mtula alisema ni vyema halmashauri kuanza kutangaza fursa zilizopo katika wilaya kwa kutumia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii ili kufanya jamii kuweza kujua fursa zilizopo ndani ya wilaya yetu.

Aliendelea kusema kuwa umeme umeenea katika maeneo mbali mbali ya wilaya ya Tunduru hali inayowezesha upatikanaji wa huduma ya umeme na wananchi kuweza kuanzisha viwanda hata maeneo ya kijiji kwa kule maeneo ambayo serikali imeshapeleka umeme.

Meneja TANESCO wilaya alitolea mfano wa mashine za kukoboa mpunga wilaya Tunduru ambazo kwa asilimia kubwa zipo katika tarafa ya mjini na kusema kuwa mashine hizi zinaweza kusimikwa pia vijijini kwa sababu umeme umefika maeneo mengi, serikali inaendelea kufunga umeme katika vijiji ambavyo havikuwa katika mpango umeme vijijini  awamu ya pili,  na barabara imeshafunguka hivyo kurahisha usafirishaji wa bidhaa hiyo.

Na kwa upande wa kaimu Afisa Madini wilaya Ndg Teddy Mataka alisisitiza kuwa Tunduru ina madini ya vito ambayo hupatikana tuu Tunduru katika nchi nzima ya  Tanzania  na pia kuna madini ya shaba  (copper), na wajibu wa Halmashauri kushirikiana na taasisi za Umma, sekta binafsi kuona kuwa fursa hizi tunatangaza na kuvutia wawekezaji kuja kuwekeza katika madini yetu.

Wajumbe  wa baraza la biashara walisisitiza elimu kutolewa kwa wafanyabiashara wadogowadogo na vikundi vya wajasiriamali ili kuweza kuhakikisha kuwa baraza hili ilinasimama na kufikia malengo ya serikali  ya kufikia uchumi wa viwanda ifikapo 2025 na agizo la viwanda 100 kwa kila mkoa linafanikiwa.

Hata wajumbe walisisitiza juu ya utwaaji wa ardhi na umilikaji ili waweze kutumia hati hizo katika kuomba mipoko katika taasisi za kibenki, na ujenzi wa hosteli kwa ajili ya wanafunzi kutokana na shule nyingi za sekondari za kata hazina hosteli hivyop wanafunzi kuhangaika makazi.


Matangazo

  • MKOPO WA HAZINA KWA WATUMISHI WA UMMA FUNGU 82N2 March 25, 2025
  • TANGAZO LA KUJIUNGA NA JESHI LA KUJENGA TAIFA KWA UTARATIBU WA KUJITOLEA October 01, 2024
  • TANGAZO LA MNADA WA HADHARA December 12, 2024
  • ORODHA YA MAJINA YA WANAOTAKIWA KUSHIRIKI USAILI WA AJIRA YA MUDA YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KATIKA WILAYA YA TUNDURU January 12, 2025
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA ROBO YA KWANZA CHA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKATABA WA LISHE KATA NA WILAYA CHAFANYIKA TUNDURU.

    November 18, 2025
  • KAMATI YA LISHE Tunduru Yajadili Mikakati Ya Kuimarisha Afua Za Lishe Katika Jamii.

    November 13, 2025
  • DC MASANJA AKAGUA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAJI MSINJI, ATAKA UKAMILISHWE HARAKA

    October 24, 2025
  • DC MASANJA ATOA WITO WA AMANI KWENYE UCHAGUZI, AENDELEA KUPIGA VITA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI TUNDURU.

    October 23, 2025
  • Ona Zote

Video

RC RUVUMA AWAPA POLE WANANCHI AMBAO NI MAJERUHI WA MGOGORO BAINA YA WAFUGAJI NA WAKULIMA TUNDURU
Video Nyingine

viunganishi vya Haraka

  • MATOKEO YA MITIHANI
  • Mkataba wa huduma kwa Mteja
  • muongozo wa Tehama
  • Ijue Sheria ya Umiliki wa Ardhi ya Mwaka 1999
  • Kanuni za Kudumu za Halmashauri ya Tunduru

Tovuti linganifu

  • Tovuti Kuu ya Rais - IKULU
  • Ofisi ya Rais - UTUMISHI
  • Ofisi ya Rais - TAMISEMI
  • Idara Kuu ya Takwimu
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Idara ya Habari Maelezo

wasomaji mbalimbali Duniani

world map hits counter

Idadi ya wasomaji

free HitCounter

Ramani

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Tunduru

    Anuani ya Posta: 275, TUNDURU

    Simu: + 255-025-2680004

    Simu ya Nununu:

    Barua Pepe: info@tundurudc.go.tz

Anuani nyingine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Kituo

Hakimiliki©2019 Halmashauri ya Wilaya Tunduru.Haki zote zimehifadhiwa.